SONONA/KUSHUKA MOYO
SONONA (DEPRESSION) SI HISIA TU. By Bernadether Bwire " Depression is a prison where you are both a prisoner and a cruel jailer." ~ Anushka Sharma "... It's like someone turned off the light inside my head...Like always the world around me loses focus and I'm trying to make sense out of it". ~Shaheen Bhatt. Katika maisha kuna nyakati binadamu tunapitia ambapo tunahisi, kuiona na kuifikiria Dunia kama giza nene. Kutokuona muelekeo wa maisha, kutokuhisi hamu ya kufanya chochote na pia kuona hakuna maana ya kuendelea kuishi duniani. Katika nyakati hizi mtu hutawaliwa na mawazo hasi ambayo yakizidi huweza mfanya mtu ajiue. Mawazo hayo hasi huongeza kudhoofika kwa moyo kwani mawazo au fikra hujawa mambo mabaya tu yaliyomtokea mtu, yanayomtokea na pia yatakayomtokea mtu. Mara nyingine si kweli kwamba mtu hukutwa na mambo haya mabaya bali katika nyakati hizi akili ya utambuzi huzibwa na mawazo hasi hivyo kusababisha mtu ashindwe kabisa kuona mwanga katika...